Serikali

Nembo ya Taifa la Tanzania

Serikali (kutoka Kiajemi سرکاری, serkari, mamlaka) ni watu na taasisi ndani ya jamii hasa dola vyenye mamlaka ya kutawala na kufanya maazimio kwa wote katika eneo fulani.

Serikali inatunza na kutekeleza sheria, kanuni na miongozo na kuendesha shughuli muhimu za umma.

Shabaha kuu ya serikali ni kutunza amani na usalama wa raia katika jamii.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search